Friday, May 24, 2013
TAIFA STARS MCHANA WAITWA IKULU KUTETA NA RAIS
Taarifa ambazo Lenzi ya Michezo imezipata zinasema Taifa stars imeitwa na Rais leo mchana kula chakula cha mchana paamoja na mambo mengine ambayo yatafahamika baadae.
Stars asubuhi imefanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume ikiwa na wachezaji 21 kwani Mwinyi Kazimoto aliumia mguu na Salum Abubakar amefiwa na baba yake mlezi hivyo amekwenda kuhudhuria msiba huo
NZERA KITANO REDD'S MISS KIBAHA 2013
Katikati Redds Miss Kibaha Nzera Kitano , kushoto
mshindi wa pili Ester Albert na kulia ni Rachel Joh ambaye ni mshindi wa tatu.
Na Ripota Wetu, Kibaha
ALIYEKUWA mshiriki namba 6
katika shindano la kumsaka Redds Miss Kibaha 2013 Nzera Kitano ameibuka kua Redds Miss Kibaha 2013
katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Conteainer Kibaha Maili Moja mkoani Pwani Mei 17 mwaka
huu
Nzera ambae alionekana kuwa
mchezi tangu mwanzo wa shindano aliweza kupenya katika hatua ya nusu fainali
ambapo aliingia katika warembo watano bora kati ya washiriki 10 waliokuwa
wakishindana kuwania taji hilo.
Aidha kwa ushindi huo Nzera amepata zawadi ya fedha taslimu
sh.300,000 pia amepa ofa ya kwenda kuchagua vipodozi na mapambo ya aina
mbalimbali katika duka la Shear Illusion lilipo Mlimani City pamoja na
king’amuzi kutoka kampuni ya Multichoice ambapo atafungiwa bure.
Mshindi wa pili ni Ester
Albert ambaye amepata fedha taslimu kiasi cha sh.200,000 pia atapata ofa ya
kulipiwa ada ya shule au kutafutiwa kazi na mdau ambaye hataki kutaja kwenye
vyombo vya habari.
Mshindi wa tatu ni Rachel
John aliyepata fedha taslimu sh. 150,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Sylvia
John huku nafasi ya tano ilikwenda kwa Beatrice Bahaya.
Kwa ushindi huo warembo wote
watano wamepata nafasi ya kwenda kushiriki kwenye shindano la Redds Miss Pwani
watakakochuana na warembo wa Bagamoyo kuwania tiketi ya kwenda kushiriki katika
shindano la Kanda ikiwa ni katika kuwania tiketi ya shindano la taifa.
Shindano hilo limeandaliwa na
Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO) na kudhaminiwa na
Redds Miss Kibaha
ilidhaminiwa na Tanzania Distilleries Konyagi kupitia kinywaji cha Dododma
Wine, Redds Premium Cold, Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Media
Group |(MMG), Aco Catering & Servises, Pr Studio, ASET ,Santorine Holiday
Resort na Amazon Night Club.
Bendi ya Muziki wa dansi ya
Mashujaa ilitumbuiza na kuwachengua mashabi wa urembo wa mkoa wa Pwani.
CHEKI MCHUMBA WA NEY WA MITEGO A.K.A MAMA KIJACHO ALIVYO MREMBO AKIWA PENY WA DIAMOND PLATNUM DAR LIVE
| Diamond akisukuma kichwa cha Ney na mchumba wake ili wabusiane |
| Peny na Mchumba wake Ney |
RAIS KIKWETE ATHIBITISHIA UMMA KWAMBA PSPF IKO IMARA NA HAITAKUFA
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.
Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya
Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake. Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya
kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma. Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na
una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na
salama katika uwekezaji . Aliongezea kwa
kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye
baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na
kudai sio kufilisika tena
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa
Pensheni wa PSPF ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr.
Rehema J. Nchimbi kuhusu shughuli za Mfuko na fursa zilizopo kwa watanzania
hususani mikopo ya nyumba na mafao ya aina mbalimbali ikiwemo fao la
Ujasiliamali na Elimu.
BFT YAOMBA WADHAMINI
Na
Elizabeth John
KOCHA wa
timu ya taifa ya ngumi, Remmy Ngabo, ameitaka serikali na wadau wa ngumi nchini,
kujitolea kudhamini kambi ya mabondia 16 ambao
wanajiandaa na mashindano ya Majiji yanayotarajia kufanyika Julai 1 hadi 7
mwaka huu, jijini Mwanza.
Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika Juni 20 hadi 25,
kutokana na kutokuwa na maandalizi ya kutosha, wamelazimika kusogeza mbele
tarehe ya kufanyika kwa mashindano hayo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, alisema mabondia hao
kwasasa wanaendelea na mazoezi ya kujifua katika uwanja wa Taifa wa Ndani
jijini Dar es Salaam kwaajili ya maandalizi ya michuano hiyo.
“Mabondia wapo katika hali ngumu ya maandalizi hivyo wadau wa
mchezo huu tunawaomba wajitokeza kudhamini maandalizi haya,” alisema.
Alisema mashindano hayo ya Majiji ni maandaliazi ya kuwaweka sawa
mabondia kwaajili ya mashindano ya Afrika na Olimpiki ambayo yanatarajia
kufanyika hivi karibuni yakishirikisha mataifa mbalimbali.
Afande Sele kuachia albamu ya ‘Amani na Upendo’
Na Elizabeth John
MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya
nchini ambaye anauwakilisha mkoa wa Morogoro, Seleman Msindi ‘Afande Sele’
ameachia albamu yake mpya inayojulikana kwa jina la ‘Amani na Upendo’.
Akizungumza na Habari Mseto jijini
Dar es Salaam, alisema licha ya soko la mauzo ya albamu kusuasua hatojali
mauzo mabaya kwakuwa lengo lake ni kuelimisha jamii na sio kupata maslahi.
“Sitofikilia soko kama litalipa au
vipi ninachohitaji ni kuwapa elimu watanzania, mashabiki wategemee kununua
albamu hiyo kwa bei rahisi,” alisema.
Alisema anaomba mashabiki waipokee
vizuri kazi hiyo na kwamba ina jumla ya nyimbo 10 ambazo zote zimefanya vizuri
katika soko hilo.
Afande sele alizitaja baadhi ya
nyimbo ambazo zipo katika albamu hiyo kuwa ni Kingdom, Karibu Morogoro, Karata
Dume na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika soko hilo.
Wednesday, May 22, 2013
MAONI YA CARTHBERT KAJUNA KUHUSU TAALUMA YA UANDISHI WA HABARI NDANI YA MAGAZETI TANDO/MITANDAO YA KIJAMII
![]() |
| Kajunason |
Watu wengi
kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila
kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo
limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko
la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).
Hatukatai kuja kwa magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook na mingine mingi.
Sina nia ya kumsema mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari hizi zote zina misingi na miiko yake.
Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na ukiisoma utakuwa unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.
Vile vile ni vizuri vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, ‘ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA NDANI’ nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?
Maana unapoandika habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini huyo aliyekamatwa ni mwizi.
Naomba tufike mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.
Napenda kuwapongeza wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti ikiwemo kutoa habari kwa njia ya ‘kufundisha masuala ya urembo, mapishi, kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua kuandika habari zao binafsi.
Nayasema yote hayo kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.
Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.
Asanteni sana kwa kusoma.
Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna
www.kajunason.blogspot.com
Hatukatai kuja kwa magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook na mingine mingi.
Sina nia ya kumsema mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari hizi zote zina misingi na miiko yake.
Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na ukiisoma utakuwa unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.
Vile vile ni vizuri vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, ‘ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA NDANI’ nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?
Maana unapoandika habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini huyo aliyekamatwa ni mwizi.
Naomba tufike mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.
Napenda kuwapongeza wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti ikiwemo kutoa habari kwa njia ya ‘kufundisha masuala ya urembo, mapishi, kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua kuandika habari zao binafsi.
Nayasema yote hayo kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.
Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.
Asanteni sana kwa kusoma.
Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna
www.kajunason.blogspot.com
MBUNGE LUKUVI AMPONGEZA RAIS KIKWETE KWA UJENZI WA BARABARA YA IRINGA- DODOMA- live
| Rais Kikwete akisalimiana na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilolo Sety Moto leo |
| Wakurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Iringa vijijini wakiwa katika uwekaji wa jiwe la msingi barabara ya Iringa - Dodoma leo eneo la Migoli Mtera |
WATUMISHI WA MAHAKAMA KUU KANDA YA IRINGA WATEMBELEA BWAWA LA MTERA IRINGA
| Watenda kazi katika mahakama kuu kanda ya Iringa wakitazama samaki walioanikwa kando kando ya bwawa la Mtera eneo la wavuvi mchana wa leo |
| Jaji kiongozi wa mahakama kuu kanda ya Iringa Mh. akiwa na kaimu msajili wa mahakama hiyo mhe. Rehema Mkuye Godfrey Isaya wakitazama |
SUMA MNAZARETI AHOJI 'TUPO WANGAPI'
Na Elizabeth John
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Suma Mnazareti
amesema
anatarajia kuachia kibao chake kipya hivi karibuni
kinachokwenda
kwa jina la ‘Tupo wangapi’.
Akizungumza jijini Dar es Salaam,Suma alisema katika
kibao hicho
ameshirikiana na msanii nyota wa muziki huo kutoka katika
kundi
la Tip Top Conection yenye maskani yake Manzese Dar es
Salaam,
Khalid Ramadhan ‘Tunda Man’.
“Unajua kila msanii ana mashabiki wake hivyo naamini
kutokana
na kufanya kazi na msanii huyo ninaimani kibao changu
kitapokelewa vizuri na mashabiki wa tasnia ya muziki
huo,”.
alisema Suma Mnazaleti.
“Nashukuru kazi zangu zinapokelewa vizuri na mashabiki
kitu
ambacho kinaniongeza uwezo wa kuendelea kuandaa kazi
nyingi
ili kuendelea kufurahisha jamii pamoja na kuelimisha
kupitia fani
hii,” alisema.
Alisema amekuwa akiumiza kichwa kila siku kwa ajili ya
kutengeneza vitu vizuri vyenye ujumbe kwa jamii lengo
lake likiwa
ni kutoka kimaisha kupitia muziki.
TSN SUPERMARKET YAJIPANGA KUIMARISHA HUDUMA ZAKE KWA NJIA YA MITANDAO YA KIJAMII
| Mkurugenzi Usambazaji wa TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman akionesha sabuni ya maji aina ya Pufy zinazouzwa na maduka hayo. |
Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowa (kushoto) na Mkurugenzi wa Usambazaji TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman wakiangalia aina ya juisi ya Lucozade Orange inayouzwa na maduka hayo.
| Lango kuu la kuingilia TSN Supermarket Tegeta, Dar es Salaam. |
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijamii wa Bongamx Media Limited, Frank Mgoyo, akielezea makubaliano na TSN Supermarket ya kutangaza bidhaa wanazouza kwenye mtandao huo.
| Meneja wa Duka la TSN Supermarket Tegeta,Godbless Massawe, akifuatilia mahesabu katika duka hilo. |
Mfanyakazi wa TSN Supermarket Tegeta, Shariffa Mbonde (kulia) akimhudumia mteja leo asubuhi katika duka hilo.
Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowa (kulia) akijadiliana na Mkurugenzi wa Usambazaji TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman jinsi ya kuboresha biashara kwa kutangaza kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Gongamx Media Limited.
YOUNG KILLER AIPONGEZA SERIKALI
Na Elizabeth John
MKALI wa muziki wa
kizazi kipya nchini, Young Killer ameipongeza serikali kwa kuamua kurudia kutoa
upya matokea ya kidato cha nne ya mwaka jana.
Akizungumza jijini Dae es Salaam, Young Killer
alisema wanafunzi wengi waliohitimu mwaka jana walikua hawana imani na matokeo
hayo, hivyo haya yeye atafarijika akiona matokeo yamerudiwa upya.
MAKAMU WA RAIS; SERIKALI IKO TAYARI KUSHIRIKIANA NA WASOMI
Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Rais Dk. Mohammed
Gharibu Bilal amesema Serikali iko tayari kushirikiana na Wasomi nchini katika
tafiti mbailimbali wanazofanya ili ziweze kuliletea Taifa maendeleo.
Akizungumza na wandishi wa
habari jijini Dar es Salaam, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya nane ya Vyuo
Vikuu vya Elimu ya Juu, Dk. Bilal, alisema maonesho hayo yanalengo la kuonesha
juhudi zinazofanywa na vyuo hivyo.
Alisema lengo la serikali kufanya
hivyo ni kuona tafiti zinazofanywa na vyuo hivyo vinaleta tija katika kumaliza matatizo
yanayoikabili jamii.
“Nafurahi kuwa hapa
kushuhudia maendeleo yaliyofikiwa na vyuo
hususan katika elimu ya juu, sayansi na teknoloji”alisema Dk. Bilal.
Dk. Bilal alisema Mpango wa
maendeleo wa serikali wa miaka mitano ambao umezinduliwa mwaka 2011 na
kukamilika mwaka 2016 moja ya eneo inalolenga ni elimu ya ubunifu.
Aidha, serikali itaendelea
kuwekeza kwenye sekta ya elimu ya juu, siyansi na teknolojia ambapo pia
itashirikiana na sekta binafsi kwa ajili ya manufaa ya jamii.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa
‘Globle Education Link’ Abdulmalik Mollel, alisema wazazi wanapaswa kujiandaa
mapema katika kuwatafutia watoto wao nafasi za elimu ya juu mapema na si
kusubiri hadi watangaziwe matokeo ya kidato cha nne na sita.
Alitoa wito kwa wazazi
kuutumia mtandao wao ambao ni mahususi katika kuwatafutia wanafunzi vyuo vya
elimu ya juu vya ndani na nje ya nchi.
Mollel alisema hadi sasa
mtandao huo umefanikiwa katika kuwatafutia vyuo wanafunzi 700 hadi 800 tangu
ulipoanzishwa mwaka 2006.
MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS
Mechi
hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco
kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco.
Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.
Bennett
atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi
msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa
akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.
Kamishna
wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa
waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na
Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma
ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na
Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 23 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 23 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 25 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume
Mei 26 Saa 3 asubuhi Uwanja wa Karume
MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari.
Mkutano huo utafanyika kesho (Mei 23 mwaka huu) saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
KUNYWA MAJI NA JUISI YA LIMAU ASUBUHI NI KINGA KUBWA KATIKA MWILI WA BINADAMU.
TUMEZOEA
kuanza siku kwa kunywa vinywaji moto kama vile kahawa au chai na hii
imekuwa ndiyo desturi ya maisha ya watu wengi duniani.
Lakini siyo
lazima kuanza siku yako kwa kunywa vinywaji hivyo, ambavyo tafiti nyingi
zimeonesha chai na kahawa vikitumiwa kupita kiasi vinaweza kuwa na
athari kwa mtumiaji.
KATIKA
kuangalia njia mbadala na bora ya kufungua kinywa na kuanza siku
vizuri, imebainika kuwa glasi moja ya maji ya uvuguvugu
yaliyochanganywa na juisi ya limau kipande kimoja, yana faida kubwa
mwilini na yanafaa kutumiwa kama kifungua kinywa asubuhi.
Zifuatazo ni baadhi ya faida kubwa za kunywa maji kwa kuchanganya na juisi ya limau asilia kama zilivyoanishwa na kuthibitishwa na tafiti mbalimbali za kisayansi:
HUSAIDIA USAGAJI CHAK
Zifuatazo ni baadhi ya faida kubwa za kunywa maji kwa kuchanganya na juisi ya limau asilia kama zilivyoanishwa na kuthibitishwa na tafiti mbalimbali za kisayansi:
HUSAIDIA USAGAJI CHAK
FLAVIANA MATATA ASHIRIKI MISA YA KUMBUKUMBU YA AJALI YA MV BUKOBA
Flaviana
Matata akiwasha mshumaa katika kaburi la Mama yake mzazi aliyefariki
dunia katika ajali ya Meli ya Mv Bukoba, ikiwa ni miaka 17 tangu
ilipotokea ajali hiyo ilipotokea. Flaviana aliwasha mshumaa huo ikiwa ni
ishara ya kuomboleza akiungana na ndugu jamaa na marafiki waliopoteza
ndugu zao katika ajali hiyo, ambapo shughuli hiyo imefanyika leo katika
Makaburi ya Igoma, jijini Mwanza, walikozikwa baadhi ya marehemu
waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
Flaviana
Matata akishirikiana na ndugu, jamaa na marafiki na baadhi ya
waombolezaji waliopoteza ndugu zao katika ajali ya Meli ya MV Bukoba,
wakiwasha mishumaa kwa pamoja ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka, wakati wa
Ibada maalum ya kumbukumbu ya ajali hiyo.
Flaviana
Matata akiwa na Baba yake mzazi na ndugu, jamaa na marafiki katika Misa
ya maombelezo Ajali ya MV Bukoba. Misa hiyo imefanyika leo, Igoma
Jijini Mwanza.
Flaviana
Matata akiwasili ofisini kwa Projest Samson Kaija, ambaye ni General
Manager wa Marine Services Company Ltd, ambao hushirikiana naye katika
maombolezo ya Ajali hiyo ambapo mwaka jana aliwapa msaada wa maboya ya
kuokolea maisha.
SIKIA HAYA YA RUVUMA: WANAKIJIJI WAFURAHIA KUONA UMEME KWA MARA YA KWANZA TOKA KUUMBWA KWA DUNIA.
| Vifaa vya Umeme Jua. |
Na Steven Augustino, Tunduru
WAKAZI wa
Kijiji cha Tinginya, tarafa ya Nakapanya Wilaya ya Tunduru mkoani
Ruvuma, wamelipuka kwa furaha baada ya kupata umeme kwa mara ya kwanza
tangu dunia iumbwe kijini kwao.
Kwa namna ya pekee wakazi hao, wameipongeza
Serikali kwa kuwafungia Mfumo wa Umeme Jua (SOLA) katika Zahanati yao na
kueleza kuwa mradi huo utawakomboa wanawake ambao kwa muda mrefu walikuwa
wakijifungua wakiwa gizani.
Kwa nyakati tofauti, wakazi hao wakiongozwa na Fatuma Mapila na Aliahad Abdalahman ambao walikuwa wamepeleka mtoto wao kwa ajili ya matibabu na Muuguzi wa Zahanati hiyo, Grolia Lup
TIKETI ZA ELEKRONIKI KUANZA KUTUMIKA UWANJA WA TAIFA
Sehemu ya umati wa wapenzi wa soka wakishuhudia mechi ya watani w3a
jadi Yanga na Simba Jumamosi iliyopita, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam. (PICHA NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)
SERIKALI imeandaa utaratibu wa kutumia tiketi za elektroniki kwa wapenzi wa soka watakaokuwa wanaingia kushuhudia mechi mbalimbali kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Akielezea bungeni leo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amosi Makalla, alisema kuwa tiketi hizo zitaanza kutumika kwa majaribio wakati wa mechi za kirafiki zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
Alisema kuwa matumizi ya tiketi za kieletroniki zitasaidia sana kudhibiti mapato kwenye Uwanja wa huo.
SERIKALI imeandaa utaratibu wa kutumia tiketi za elektroniki kwa wapenzi wa soka watakaokuwa wanaingia kushuhudia mechi mbalimbali kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Akielezea bungeni leo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amosi Makalla, alisema kuwa tiketi hizo zitaanza kutumika kwa majaribio wakati wa mechi za kirafiki zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
Alisema kuwa matumizi ya tiketi za kieletroniki zitasaidia sana kudhibiti mapato kwenye Uwanja wa huo.
WATU WA MBEYA HAWAKOMI: SHUHUDIA WANANCHI WA MLIMA NYOKA MBEYA WALIVYO GOMBANIA MAFUTA BAADA YA GARI LA MAFUTA KAMPUNI YA LAKE OIL KUPINDUKA
WAKAZI WA MLIMA NYOKA MKOANI MBEYA WAKIWA NA PILIKA KUELEKEA KUCHOTA MAFUTA BAADA YA GARI HILO KUPINDUKA.
SHUHUDIA WAKAZI WA MLIMA NYOKA WAKIWA WANAGOMBANIA MAFUTA
GARI LA KAMPUNI YA LAKE OIL BAADA YA KUPINDUKA
KILA MKAZI YUPO BIZE NA MAFUTA
PICHA NA MBEYA YETU
Subscribe to:
Posts (Atom)
























