Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, May 24, 2013

SPLASH WAA NA IDENTTTY CARD


TAIFA STARS MCHANA WAITWA IKULU KUTETA NA RAIS


TIMU ya Taifa 'Taifa stars" ambayo ipo kambini kujiandaa na mchezo wa marudiano na Morocco wa kutafuta kufuzu fainali za dunia 2014 nchini Brazil imealikwa Ikulu kula chakula cha mchana leo.

Taarifa ambazo Lenzi ya Michezo imezipata zinasema Taifa stars imeitwa na Rais leo mchana kula chakula cha mchana paamoja na mambo mengine ambayo yatafahamika baadae.

Stars asubuhi imefanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume ikiwa na wachezaji 21 kwani Mwinyi Kazimoto aliumia mguu na Salum Abubakar amefiwa na baba yake mlezi hivyo amekwenda kuhudhuria msiba huo




NZERA KITANO REDD'S MISS KIBAHA 2013



Katikati  Redds Miss Kibaha Nzera Kitano , kushoto mshindi wa pili Ester Albert na kulia ni Rachel Joh ambaye ni mshindi wa tatu.
Na Ripota Wetu, Kibaha
ALIYEKUWA mshiriki namba 6 katika shindano la kumsaka Redds Miss Kibaha 2013 Nzera  Kitano ameibuka kua Redds Miss Kibaha 2013 katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Conteainer  Kibaha Maili Moja mkoani Pwani Mei 17 mwaka huu
Nzera ambae alionekana kuwa mchezi tangu mwanzo wa shindano aliweza kupenya katika hatua ya nusu fainali ambapo aliingia katika warembo watano bora kati ya washiriki 10 waliokuwa wakishindana kuwania taji hilo.

 Aidha kwa ushindi huo  Nzera amepata zawadi ya fedha taslimu sh.300,000 pia amepa ofa ya kwenda kuchagua vipodozi na mapambo ya aina mbalimbali katika duka la Shear Illusion lilipo Mlimani City pamoja na king’amuzi kutoka kampuni ya Multichoice ambapo atafungiwa bure.
 
Mshindi wa pili ni Ester Albert ambaye amepata fedha taslimu kiasi cha sh.200,000 pia atapata ofa ya kulipiwa ada ya shule au kutafutiwa kazi na mdau ambaye hataki kutaja kwenye vyombo vya habari.
 
Mshindi wa tatu ni Rachel John aliyepata fedha taslimu sh. 150,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Sylvia John huku nafasi ya tano ilikwenda kwa Beatrice Bahaya.
 
Kwa ushindi huo warembo wote watano wamepata nafasi ya kwenda kushiriki kwenye shindano la Redds Miss Pwani watakakochuana na warembo wa Bagamoyo kuwania tiketi ya kwenda kushiriki katika shindano la Kanda ikiwa ni katika kuwania  tiketi ya shindano la taifa.
Shindano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO) na kudhaminiwa na
Redds Miss Kibaha ilidhaminiwa na Tanzania Distilleries Konyagi kupitia kinywaji cha Dododma Wine, Redds Premium Cold, Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Media Group |(MMG), Aco Catering & Servises, Pr Studio, ASET ,Santorine Holiday Resort na Amazon Night Club.
Bendi ya Muziki wa dansi ya Mashujaa ilitumbuiza na kuwachengua mashabi wa urembo wa mkoa wa Pwani.

CHEKI MCHUMBA WA NEY WA MITEGO A.K.A MAMA KIJACHO ALIVYO MREMBO AKIWA PENY WA DIAMOND PLATNUM DAR LIVE



clip_image001[16]
clip_image001
Bila shaka unafahamu kuwa Nay wa Mitego ni baba mtarajiwa. Mara nyingi Nay amekuwa akiweka picha ya mpenzi wake anayetarajia kumzalia mtoto hivi karibuni lakini hujawahi kuona picha yake inayoonekana vizuri zaidi. Tazama picha hizi za shemeji/wifi yetu zilizochukuliwa kwenye show ya Nay na Diamond, Dar Live weekend iliyopita.
clip_image001[6]
Diamond akisukuma kichwa cha Ney na mchumba wake ili wabusiane
clip_image001[8]
clip_image001[10]
Peny na Mchumba wake Ney 
clip_image001[12]
clip_image001[14]

RAIS KIKWETE ATHIBITISHIA UMMA KWAMBA PSPF IKO IMARA NA HAITAKUFA


 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu  tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake.  Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma.  Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na salama katika uwekezaji .  Aliongezea kwa kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na kudai sio kufilisika tena

 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma kipeperushi cha nyumba za PSPF zinazokopeshwa kwa wanachama wa Mfuko huo, huku akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa  Mfuko huo ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea kuhusu nyumba hizo na fursa zingine zilizopo PSPF kwa Watanzania ikiwa ni pamoja na ujumbe kwa Watanzania kwamba mtu yeyote mwenye umri usiopungua miaka 18 anaweza kuwa mwanachama wa PSPF

  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema J. Nchimbi kuhusu shughuli za Mfuko na fursa zilizopo kwa watanzania hususani mikopo ya nyumba na mafao ya aina mbalimbali ikiwemo fao la Ujasiliamali na Elimu.
   Mtangazaji wa TBC Amina Mollel akikabidhi fomu ya kujiunga na PSPF kwa Meneja Masoko wa Mfuko huo Bi. Costantina Martin mala baada ya kuvutiwa na kukata shauri ya kuwa mwanachama wa Mfuko wa kwa njia ya uchangiaji wa hiari
Timu ya PSPF iliyokuwa kwenye maonyesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii wakiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wao ndugu Adamu Mayingu katikati.  Timu hiyo inastahili pongezi kutokana na uduma bora waliyokuwa wakiitoa kwa wananchi waliokuwa wakitembelea banda hilo la PSPF pale Nyerere squire Dodoma.
Wanachama wa PSPF wakipata taarifa mbalimbali ikiwapo historia ya michango yao na taarifa za uanachama.

BFT YAOMBA WADHAMINI


Na Elizabeth John


KOCHA wa timu ya taifa ya ngumi, Remmy Ngabo, ameitaka serikali na wadau wa ngumi nchini, kujitolea kudhamini kambi ya mabondia 16 ambao wanajiandaa na mashindano ya Majiji yanayotarajia kufanyika Julai 1 hadi 7 mwaka huu, jijini Mwanza.
Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika Juni 20 hadi 25, kutokana na kutokuwa na maandalizi ya kutosha, wamelazimika kusogeza mbele tarehe ya kufanyika kwa mashindano hayo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, alisema mabondia hao kwasasa wanaendelea na mazoezi ya kujifua katika uwanja wa Taifa wa Ndani jijini Dar es Salaam kwaajili ya maandalizi ya michuano hiyo.
“Mabondia wapo katika hali ngumu ya maandalizi hivyo wadau wa mchezo huu tunawaomba wajitokeza kudhamini maandalizi haya,” alisema.
Alisema mashindano hayo ya Majiji ni maandaliazi ya kuwaweka sawa mabondia kwaajili ya mashindano ya Afrika na Olimpiki ambayo yanatarajia kufanyika hivi karibuni yakishirikisha mataifa mbalimbali.
“Maandalizi mazuri ya mashindano makubwa ni haya mashindano madogo, mabondia wanatakiwa kufanya mazoezi ya kutosha ili kushiriki mashindano hayo,” alisema Kocha huyo ambaye anatambulika na Shirikisho la Ngumi Duniani (AIBA).

Afande Sele kuachia albamu ya ‘Amani na Upendo’


Na Elizabeth John

MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya nchini ambaye anauwakilisha mkoa wa Morogoro, Seleman Msindi ‘Afande Sele’ ameachia albamu yake mpya inayojulikana kwa jina la ‘Amani na Upendo’.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, alisema licha ya soko la mauzo ya albamu kusuasua hatojali mauzo mabaya kwakuwa lengo lake ni kuelimisha jamii na sio kupata maslahi.

“Sitofikilia soko kama litalipa au vipi ninachohitaji ni kuwapa elimu watanzania, mashabiki wategemee kununua albamu hiyo kwa bei rahisi,” alisema.

Alisema anaomba mashabiki waipokee vizuri kazi hiyo na kwamba ina jumla ya nyimbo 10 ambazo zote zimefanya vizuri katika soko hilo.

Afande sele alizitaja baadhi ya nyimbo ambazo zipo katika albamu hiyo kuwa ni Kingdom, Karibu Morogoro, Karata Dume na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika soko hilo.

Wednesday, May 22, 2013

MAONI YA CARTHBERT KAJUNA KUHUSU TAALUMA YA UANDISHI WA HABARI NDANI YA MAGAZETI TANDO/MITANDAO YA KIJAMII

Kajunason
Watu wengi kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).

Hatukatai kuja kwa magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook na mingine mingi.

Sina nia ya kumsema mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari hizi zote zina misingi na miiko yake.

 Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na ukiisoma utakuwa unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.

Vile vile ni vizuri vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, ‘ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA NDANI’ nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?

Maana unapoandika habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini huyo aliyekamatwa ni mwizi.

Naomba tufike mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.

Napenda kuwapongeza wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti ikiwemo kutoa habari kwa njia ya ‘kufundisha masuala ya urembo, mapishi, kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua kuandika habari zao binafsi.

Nayasema yote hayo kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.

Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.

Asanteni sana kwa kusoma.

Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna

www.kajunason.blogspot.com

MBUNGE LUKUVI AMPONGEZA RAIS KIKWETE KWA UJENZI WA BARABARA YA IRINGA- DODOMA- live


Rais  Kikwete  akisalimiana na mwenyekiti wa CCM wilaya ya  Kilolo Sety Moto leo
Wakurugenzi  wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa na Iringa  vijijini wakiwa katika  uwekaji  wa  jiwe la msingi barabara ya Iringa - Dodoma  leo eneo la Migoli Mtera
Rais Jakaya  Kikwete (kushoto) akiteta  jambo na mbunge wa  jimbo la Isimani Wiliam Lukuvi  leo

 watumishi  wa mahakama kuu kanda ya  Iringa  pia wamepata  kushiriki
.............................................................................. 

MBUNGE  wa  jimbo la Isimani wilayani  Iringa mkoani Iringa  Bw. Wiliam Lukuvi amempongeza  Rais Jakaya  Kikwete  kwa  kuwawezesha  wakazi  wa tarafa  ya Isimani kuweza  kuanza  kushuhudia mapinduzi makubwa ya  kimaendeleo kupitia mradi mkubwa  wa barabara  ya  kiwango  cha lami kutoka Iringa - Dodoma  inayopita katika   tarafa  hiyo .
 
Lukuvi  ambae ni  waziri  wa nchi  ofisi  ya  waziri  mkuu (sera na uratibu  wa  bunge) alisema  kuwa  barabara  hiyo ambayo ni ukombozi mkubwa kwa nchi  za  kusini mwa  Tanzania  ilikuwemo katika mkakati  wa kujengwa kwa kiwango  cha lami kwa kitambo  kirefu na  kila awamu  wananchi  walikuwa  wakiulizana  juu ya kuanza  kwa mradi huo.
 
Hata  hivyo  alisema  baada ya awamu  hii ya nne  chini ya  Rais Kikwete  wananchi hao  wameweza kushuhudia  majibu ya maswali yao  kwa  kuanza  kwa ujenzi huo ambao  kila mmoja anatambua  kama ni ukombozi katika  sekta ya maendeleo.
 
Waziri  Lukuvi alitoa  pongezi  hizo kwa Rais Kikwete  leo wakati akiwasalimia  wananchi  wa  jimbo  la Isimani ambao  walishiriki hafla  fupi ya Rais Kikwete  kuweka jiwe 
 
Kwa  upande  wake  Rais Jakaya  Kikwete  alisema  kuwa  mbali ya  serikali  kujipanga kwa  ujenzi  wa barabara bado lengo la  serikali ni  kuhakikisha nchi  nzima inaunganishwa kwa mtandao  wa barabara  ya lami na kuwa kazi hiyo tayari  imeanza.
 
Alisema  kuwa serikali  yake  toka  imeingia madarakani  imeendelea  kuongeza  fedha  katika mfuko  wa barabara  na kuwa lengo ni kuendelea  kuongeza  zaidi fedha katika mfuko  huo ili  kuwezesha  ujenzi  wa barabara nchini kuweza  kukamilika 
 
 Rais  Kikwete  pia amewapongeza  viongozi wa TANROADS kwa kazi nzuri  wanayoendelea  kuifanya na kwa  mbali ya kupongezwa bado hawapaswi kulewa  sifa na badala  yake  kuendeleza  jitihada za  kusimamia  kazi  hiyo kwani upo usemi unao sema kuwa mgema akisifiwa pombe huweka maji .
 
Pia  Rais Kikwete alimpompongeza  waziri wa fedha Dkt Wiliam Mgimwa kwa kuendelea  kuidhinisha  fedha kwa ajili ya miradi ya barabara hapa nchini na kuwa  bila  wizara  hiyo  kutenga bajeti  kazi hiyo ingeendelea  kuwa ngumu.

WATUMISHI WA MAHAKAMA KUU KANDA YA IRINGA WATEMBELEA BWAWA LA MTERA IRINGA


Watenda kazi katika mahakama kuu kanda  ya  Iringa  wakitazama samaki  walioanikwa kando kando ya bwawa la Mtera  eneo la  wavuvi mchana wa  leo
Kaimu msajili  wa mahakama kuu kanda  ya Iringa Mhe. Godfrey Isaya  (kushoto) akiwa na  watenda kazi  wengine  wa mahakama hiyo kando kando ya  bwawa la Mtera  Iringa  leo baada ya  kutembelea  eneo  hilo mara  baada ya  Rais Jakaya  Kikwete  kumaliza  kuweka  jiwe la msingi katika ujenzi wa barabara  ya Iringa - Dodoma
Jaji kiongozi wa mahakama kuu kanda  ya Iringa Mh. akiwa na kaimu msajili wa mahakama hiyo mhe. Rehema Mkuye  Godfrey Isaya wakitazama

SUMA MNAZARETI AHOJI 'TUPO WANGAPI'


Na Elizabeth John

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Suma Mnazareti amesema
anatarajia kuachia kibao chake kipya hivi karibuni kinachokwenda
kwa jina la ‘Tupo wangapi’.
Akizungumza jijini Dar es Salaam,Suma alisema katika kibao hicho
ameshirikiana na msanii nyota wa muziki huo kutoka katika kundi
la Tip Top Conection yenye maskani yake Manzese Dar es Salaam,
Khalid Ramadhan ‘Tunda Man’.
“Unajua kila msanii ana mashabiki wake hivyo naamini kutokana
na kufanya kazi na msanii huyo ninaimani kibao changu
kitapokelewa vizuri na mashabiki wa tasnia ya muziki huo,”.
alisema Suma Mnazaleti.
“Nashukuru kazi zangu zinapokelewa vizuri na mashabiki kitu
ambacho kinaniongeza uwezo wa kuendelea kuandaa kazi nyingi
ili kuendelea kufurahisha jamii pamoja na kuelimisha kupitia fani
hii,” alisema.
Alisema amekuwa akiumiza kichwa kila siku kwa ajili ya
kutengeneza vitu vizuri vyenye ujumbe kwa jamii lengo lake likiwa

ni kutoka kimaisha kupitia muziki.

TSN SUPERMARKET YAJIPANGA KUIMARISHA HUDUMA ZAKE KWA NJIA YA MITANDAO YA KIJAMII


Mkurugenzi Usambazaji wa TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman akionesha uimara wa sahani aina ya Luminarc zinazouzwa na maduka yao.
Mkurugenzi Usambazaji wa TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman akionesha sabuni ya maji aina ya Pufy zinazouzwa na maduka hayo.
Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowa (kushoto) na Mkurugenzi wa Usambazaji TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman  wakiangalia aina ya Ice Cream ya Kulfi katika duka la Tegeta, Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowa (kushoto) na Mkurugenzi wa Usambazaji TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman wakiangalia aina ya juisi ya Lucozade Orange inayouzwa na maduka hayo.
Lango kuu la kuingilia TSN Supermarket Tegeta, Dar es Salaam.
Mkurugenzi Usambazaji wa TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman akielezea kuhusu mikakati ya kuboresha biashara zao kwa kuzitangaza kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ili kumrahisishia mteja kujua bidhaa zinazouzwa katika maduka yao yaliyopo, Tegeta, Bamaga Mwenge, Mikocheni na Upanga Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijamii wa Bongamx Media Limited, Frank Mgoyo, akielezea makubaliano na TSN Supermarket ya kutangaza bidhaa wanazouza kwenye mtandao huo.
Meneja wa Duka la TSN Supermarket Tegeta,Godbless Massawe, akifuatilia mahesabu katika duka hilo.


Mfanyakazi wa TSN Supermarket Tegeta, Shariffa Mbonde (kulia) akimhudumia mteja leo asubuhi katika duka hilo.

Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowa (kulia) akijadiliana na Mkurugenzi wa Usambazaji TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman jinsi ya kuboresha biashara kwa kutangaza kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Gongamx Media Limited.

YOUNG KILLER AIPONGEZA SERIKALI


Na Elizabeth John

MKALI wa  muziki wa kizazi kipya nchini, Young Killer ameipongeza serikali kwa kuamua kurudia kutoa upya matokea ya kidato cha nne ya mwaka jana.
Akizungumza jijini Dae es Salaam, Young Killer alisema wanafunzi wengi waliohitimu mwaka jana walikua hawana imani na matokeo hayo, hivyo haya yeye atafarijika akiona matokeo yamerudiwa upya.
“Kiukweli wengi tunajua kwa matokeo hayo tumeonewa, mimi nitaona kweli nimefeli halali endapo matokeo ya pili yataonesha hivyo lakini kwasaivi naamini kama walinipa matokeo ya mntu mwingine,” alisema msanii huyo ambaye ni miongozi mwa wanafunzi waliohitimu kidato cha nne mwaka jana.

MAKAMU WA RAIS; SERIKALI IKO TAYARI KUSHIRIKIANA NA WASOMI



Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Rais Dk. Mohammed Gharibu Bilal amesema Serikali iko tayari kushirikiana na Wasomi nchini katika tafiti mbailimbali wanazofanya ili ziweze kuliletea Taifa maendeleo.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya nane ya Vyuo Vikuu vya Elimu ya Juu, Dk. Bilal, alisema maonesho hayo yanalengo la kuonesha juhudi zinazofanywa na vyuo hivyo.
Alisema lengo la serikali kufanya hivyo ni kuona tafiti zinazofanywa na vyuo hivyo vinaleta tija katika kumaliza matatizo yanayoikabili jamii.
“Nafurahi kuwa hapa kushuhudia maendeleo yaliyofikiwa na vyuo  hususan katika elimu ya juu, sayansi na teknoloji”alisema Dk. Bilal.
Dk. Bilal alisema Mpango wa maendeleo wa serikali wa miaka mitano ambao umezinduliwa mwaka 2011 na kukamilika mwaka 2016 moja ya eneo inalolenga ni elimu ya ubunifu.
Aidha, serikali itaendelea kuwekeza kwenye sekta ya elimu ya juu, siyansi na teknolojia ambapo pia itashirikiana na sekta binafsi kwa ajili ya manufaa ya jamii.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa ‘Globle Education Link’ Abdulmalik Mollel, alisema wazazi wanapaswa kujiandaa mapema katika kuwatafutia watoto wao nafasi za elimu ya juu mapema na si kusubiri hadi watangaziwe matokeo ya kidato cha nne na sita.
Alitoa wito kwa wazazi kuutumia mtandao wao ambao ni mahususi katika kuwatafutia wanafunzi vyuo vya elimu ya juu vya ndani na nje ya nchi.
Mollel alisema hadi sasa mtandao huo umefanikiwa katika kuwatafutia vyuo wanafunzi 700 hadi 800 tangu ulipoanzishwa mwaka 2006.

MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS


MOROCCO Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas). 

 Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett. 

 Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.

 Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda. Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia. 

 Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo; Mei 22 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 23 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 23 Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 25 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni Uwanja wa Karume Mei 26 Saa 3 asubuhi Uwanja wa Karume MKUTANO WA WAANDISHI WA HABARI Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga atakuwa na mkutano na waandishi wa habari.

 Mkutano huo utafanyika kesho (Mei 23 mwaka huu) saa 5 kamili asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF. Boniface Wambura Ofisa Habari Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

KUNYWA MAJI NA JUISI YA LIMAU ASUBUHI NI KINGA KUBWA KATIKA MWILI WA BINADAMU.


TUMEZOEA kuanza siku kwa kunywa vinywaji moto kama vile kahawa au chai na hii imekuwa ndiyo desturi ya maisha ya watu wengi duniani.

Lakini siyo lazima kuanza siku yako kwa kunywa vinywaji hivyo, ambavyo tafiti nyingi zimeonesha chai na kahawa vikitumiwa kupita kiasi vinaweza kuwa na athari kwa mtumiaji.
KATIKA kuangalia njia mbadala na bora ya kufungua kinywa na kuanza siku vizuri, imebainika kuwa glasi moja ya maji ya  uvuguvugu yaliyochanganywa na juisi ya limau kipande kimoja, yana faida kubwa mwilini na yanafaa kutumiwa kama kifungua kinywa asubuhi.

Zifuatazo ni baadhi ya faida kubwa za kunywa maji kwa kuchanganya na juisi ya limau asilia kama zilivyoanishwa na kuthibitishwa na tafiti mbalimbali za kisayansi:

HUSAIDIA USAGAJI CHAK

FLAVIANA MATATA ASHIRIKI MISA YA KUMBUKUMBU YA AJALI YA MV BUKOBA


 Flaviana Matata akiwasha mshumaa katika kaburi la Mama yake mzazi aliyefariki dunia katika ajali ya Meli ya Mv Bukoba, ikiwa ni miaka 17 tangu ilipotokea ajali hiyo ilipotokea. Flaviana aliwasha mshumaa huo ikiwa ni ishara ya kuomboleza akiungana na ndugu jamaa na marafiki waliopoteza ndugu zao katika ajali hiyo, ambapo shughuli hiyo imefanyika leo katika Makaburi ya Igoma, jijini Mwanza, walikozikwa baadhi ya marehemu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
 Flaviana Matata akishirikiana na ndugu, jamaa na marafiki na baadhi ya waombolezaji waliopoteza ndugu zao katika ajali ya Meli ya MV Bukoba, wakiwasha mishumaa kwa pamoja ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka, wakati wa Ibada maalum ya kumbukumbu ya ajali hiyo.
 Flaviana Matata akiwa na Baba yake mzazi na ndugu, jamaa na marafiki katika Misa ya  maombelezo  Ajali ya MV Bukoba. Misa hiyo imefanyika leo, Igoma Jijini Mwanza.
Flaviana Matata akiwasili ofisini kwa Projest  Samson Kaija, ambaye ni General Manager wa Marine Services Company Ltd, ambao hushirikiana naye katika maombolezo ya Ajali hiyo ambapo mwaka jana aliwapa msaada wa maboya ya kuokolea maisha.

SIKIA HAYA YA RUVUMA: WANAKIJIJI WAFURAHIA KUONA UMEME KWA MARA YA KWANZA TOKA KUUMBWA KWA DUNIA.


Vifaa vya Umeme Jua.

Na Steven Augustino, Tunduru
WAKAZI wa Kijiji cha Tinginya, tarafa ya Nakapanya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, wamelipuka kwa furaha baada ya kupata umeme kwa mara ya kwanza tangu dunia iumbwe kijini kwao.
Kwa namna ya pekee wakazi hao, wameipongeza Serikali kwa kuwafungia Mfumo wa Umeme Jua (SOLA) katika Zahanati yao na kueleza kuwa mradi huo utawakomboa wanawake ambao kwa muda mrefu walikuwa wakijifungua wakiwa gizani.

Kwa nyakati tofauti, wakazi hao wakiongozwa na Fatuma Mapila na Aliahad Abdalahman ambao walikuwa wamepeleka mtoto wao kwa ajili ya matibabu na Muuguzi wa Zahanati hiyo, Grolia Lup

TIKETI ZA ELEKRONIKI KUANZA KUTUMIKA UWANJA WA TAIFA


 Sehemu ya umati wa wapenzi wa soka wakishuhudia mechi ya watani w3a jadi Yanga na Simba Jumamosi iliyopita, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. (PICHA NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)

SERIKALI imeandaa utaratibu wa kutumia tiketi za elektroniki kwa wapenzi wa soka watakaokuwa wanaingia kushuhudia mechi mbalimbali kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Akielezea bungeni leo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amosi Makalla, alisema kuwa tiketi hizo zitaanza kutumika kwa majaribio  wakati wa mechi za kirafiki zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Alisema kuwa matumizi ya tiketi za kieletroniki zitasaidia sana kudhibiti mapato kwenye Uwanja wa huo.

WATU WA MBEYA HAWAKOMI: SHUHUDIA WANANCHI WA MLIMA NYOKA MBEYA WALIVYO GOMBANIA MAFUTA BAADA YA GARI LA MAFUTA KAMPUNI YA LAKE OIL KUPINDUKA


 WAKAZI WA MLIMA NYOKA MKOANI MBEYA WAKIWA NA PILIKA KUELEKEA KUCHOTA MAFUTA BAADA YA GARI HILO KUPINDUKA.
 SHUHUDIA WAKAZI WA MLIMA NYOKA WAKIWA WANAGOMBANIA MAFUTA
 GARI LA KAMPUNI YA LAKE OIL BAADA YA KUPINDUKA
 KILA MKAZI YUPO BIZE NA MAFUTA
 PICHA NA MBEYA YETU
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...