Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, October 9, 2010

MIKUTANO YA KIMATAIFA BENKI YA DUNIA YAANZA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI

MIKUTANO YA MWAKA YA SHIRIKA LA FEDHA LA KIMATAIFA NA KUNDI LA BENKI YA DUNIA YAANZA.
Mikutano ya mwaka ya Bodi ya Magavana ya Shirika la fedha la Kimataifa na kundi la Benkiya Dunia kwa mwaka 2010 imeanza leo mjini Washington D.C. Kilele cha mikutano hiyo kitakuwa tarehe 8 - 10, mwezi Octoba 2010.
Bodi ya Magavana wa Shirika la Fedha la kimataifa ( Mfuko) na Bodi ya Magavana wa kundi la Benki ( Benki ) kwa kawaida hukutana mara moja kwa mwaka kujadili kazi za Taasisi zinazowahusu. Mikutano hii ya mwaka huwa inafanyika mwezi Septemba hadi Octoba, hufanyika mjini Washington kwa miaka miwili mfululizo na kwa mwaka wa tatu hufanyika kwa nchi mwanachama.
Uzinduzi wa Mikutano hii ya Bodi ya Magavana ulifanyika Savannah, Georgia, Amerika mwezi Machi mwaka 1946. Na mikutano ya kwanza ya mwaka ilifanyika mjini Washington mwaka1946.
Mwaka huu,Mikutano ya mwaka itaambatana pamoja na mikutano ya kimataifa ya kifedha na kamati za fedha, Kamati za maendeleo, kundi la nchi kumi, kundi la nchi ishirini na nne, na makundi mbalimbali ya nchi wanachama.
Aidha mwisho wa mikutano hii, Shirika la fedha la kimataifa, kamati ya mambo ya fedha, Kamati ya maendeleo pamoja na makundi mengine watapata nafasi ya kuwasiliana na kutoa mapendekezo yao.
Mikutano hii ya mwaka itaunganisha siku za utangulizi kabla ya ufunguzi rasmi kipindi ambacho Magavana watakitumia kwa kuzungumzia masuala ya kibiashara na kushauriana.Vilevile katika Mikutano hii ya mwaka, Bodi ya Magavana huwa inafanya maamuzi ya ni vipi mambo ya Fedha ya kimataifa yanapaswa kuwa na kukubaliana kuhusu maazimio husika.
Mikutanoya mwaka inakuwa na mwenyekiti ambaye ni Gavana wa Benki na wa Mfuko, na uenyekiti huo unakuwa ni wa kupokezana kati ya wanachama kila mwaka. Kila baada ya miaka miwili inachagua Mkurugenzi mtendaji. Kila mwaka wanachama wapya wowote wanakaribishwa katika Benki na mfuko.
Kwa sababu Mikutano hii ya mwaka inakusanya idadi kubwa ya wanachama kutoka nchi mbalimbali, hivyo shirika la fedha la kimataifa na kundi la Benki ya Dunia inatoa nafasi ya kuwapatia ushauri mkubwa na mdogo, kwa mpangilio wa kuwa na utaratibu maalumu au kutokuwa na utaratibu maalumu alimradi hawavurugi mpangilio uliopo.
Semina mbali mbali zinafanyika wakati wa mikutano na zinaaendeshwa na wafanyakazi wanachama kwa waandishi wa habari.Programu za Mikutano ya mwaka zimetengenezwa kwa kuzingatia matakwa ya sekta binafsi, wajumbe kutoka Serikalini na maafisa wakuu wa Mabenki na watumishi wa Mfuko.
Mikutano ya mwaka nje ya Amerika kuanzia mwaka
1947—2009
Mwaka
Nchi
1947
London
1950
Paris
1952
Mexico City
1955
Istanbul
1958
New Delhi
1961
Vienna
1964
Tokyo
1967
Rio de Janeiro
1970
Copenhagen
1973
Nairobi
1976
Manila
1979
Belgrade
1982
Toronto
1985
Seoul
1988
Berlin
1991
Bangkok
1994
Madrid
1997
Hong Kong
2000
Prague
2003
Dubai
2006
Singapore
2009
Istanbul
Magavana wa mikutano hiyo ni Mawaziri wa fedha kutoka nchi mbalimbali, Magavana wa Benki kuu na Makatibu wa kuu wa Wizara za fedha.
Mpaka sasa karibu nchi zote zimeisha wasili katika mikutano hiyo.


Imetolewa na:
Ingiahedi Mduma
Msemaji Mkuu
Wizara ya Fedha na uchumi
Washington D.C
4/10/2010

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...