Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, April 11, 2014

Tumebahatisha kuifunga Kagera Sugar-Ngassa



Mrisho Ngassa (kulia) akiwa na wachezaji wenzake Simon Msuva na Didier Kavumbagu wakishangilia bao lao la kwanza dhidi ya Kagera lililofungwa na Kavun\mbagu (kati)
WINGA hatari wa Yanga, Mrisho Ngasa ameimwagia sifa timu ya Kagera Sugar huku akiweka wazi kwamba timu yake imebahatisha kupata ushindi dhidi ya timu hiyo katika mechi yao ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa juzi.
Ngasa aliyasema hayo katika mahojiano mara tu baada ya mechi hiyo raundi ya 24 waliyoshinda 2-1 huku akitoa pasi ya mwisho ya goli la kwanza lililofungwa na mshambuliaji Mganda Hamis Kiiza na kupika pia la pili lililopachikwa na straika Mrundi Didier Kavumbagu.
“Ilikuwa mechi ngumu sana, Kagera ni wazuri na walitawala mchezo hasa kipindi cha pili, ni bahati tu iliyotusaidia wasipate magoli mengi zaidi,” alisema Ngassa.
“Tuna kazi kubwa ya kufanya hasa katika mechi zilizobaki ukizingatia bado hatujacheza dhidi ya Simba ambao mara nyingi wamekuwa wakitukamia sana.”
Ngasa, mchezaji wa zamani wa Kahama United, Kagera Sugar, Simba na Azam FC, alianza katika mechi ya juzi kabla ya kumpisha mshambuliaji wa zamani wa Mtibwa Sugar, Hussein Javu katika dakika ya 63.
Winga huyo tegemeo katika kikosi cha Mholanzi Hans van der Pluijm cha Yanga, alifunga goli la kwanza katika ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Kagera Sugar katika mechi yao ya mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Kagera Oktoba 12 mwaka jana
NIPASHE

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...