Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Saturday, July 5, 2014

UZINDUZI WA ATM ZA SELCOM ZAFANA KATIKA VIWANJA VYA SABASABA

Meneja miradi wa kampuni ya Selcom Wireless, Gallus Runyela kulia akiwaelekeza kina mama waliotembelea kutoa pesa wakati wa uzinduzi wa mashine ya ATM ya kampuni hiyo ambazo zinatoa  pesa kwa kutumia mitandao mbalimbali ya simu kama M-pesa,tigo pesa,Airtel Money, walipo tembelea katika maonyesho ya 38 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu JK Nyerere  kushoto ni Ester Kariwa na Joyce Mtema picha na mpiga picha wetu
Mmoja ya wateja waliotembelea banda la kampuni ya Selcom Wireless, Bi,Joriet Benjamin akichukuwa fedha zake katika ATM mashine mpya za kampuni hiyo wakati wa
maonyesho ya 38 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu JK Nyerere
Wafanyakazi wa Selcom kampuni ya Wireless, wakiwa katika banda lao wakati wa
maonyesho ya 38 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu JK Nyerere kutoka kushoto ni Juma Mgori Meneja ukuzaji biashara na masoko,Ofisa Mauzo Ally Mbaga na Meneja miradi wa kampuni hiyo Gallus Runyela

ATM mpya na za kisasa za selcom zawa kivutio kikubwa kwa kampuni ya selcom ambayo imekuwa ikijihusisha na utoaji wa malipo mbalimbali kama vile ving'amuzi na luku mwaka huu imezindua huduma yake mpya ya ATM ambazo zitakuwa zinatoa pesa kwa kutumia mitandao kama Mpesa,Tigo pesa,Airtel Money, na Easy pesa ATM hizo zimevuta hisia nyingi kwa watanzania baada ya kuziona kwa mara ya kwanza katika banda la Selcom na kushudia ATM hizo mpya na za kwanza nchini kutumika kutoa pesa kwa njia ya simu za mkononi
Meneja miradi wa kampuni ya Selcom Wireless, Gallus Runyela kulia akiwaelekeza Goerge Vupembe jinsi ya mashine zinavyofanya kazi
Ofisa Mauzo wa Kampuni ya Selcom Wireless  Ally Mbaga  kushoto akifurahia jambo na mteja, Bi, Rose Mombo aliyekuja kutoa pesa katika mashine ya ATM ya kampuni hiyo




Mtaalamu wa ufundi wa mashine za ATM za Selcom, Maful Awadhakitoa maherekezo ya jinsi ya kutumia mashine hizo
Meneja ukuzaji biashara na masoko  kampuni ya Selcom Wireless Juma Mgori akionesha mashine hiyo

Mtaalamu wa ufundi wa mashine za ATM za Selcom, Maful Awadh akiwa katika moja ya mashine hizo zilizozinduliwa katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es salaam
Meneja ukuzaji biashara na masoko
Juma Mgori akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mashine za ATM za kampuni hiyo kwa ajili ya kutolea fedha
kutumia mitandao kama Mpesa,Tigo pesa,Airtel Money, na Easy pesa ATM hizo zimevuta hisia nyingi kwa watanzania baada ya kuziona kwa mara ya kwanza katika banda la Selcom na kushudia ATM hizo mpya na za kwanza nchini kutumika kutoa pesa kwa njia ya simu za mkononi
Meneja miradi wa kampuni ya Selcom Wireless, Gallus Runyela kulia akihojiwa na waandishi wa habari kuhusu mashine hizo za ATM
wakati wa
maonyesho ya 38 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu JK Nyerere

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...