Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, August 7, 2014

WHO kuamua Ebola janga la dunia


Mhudumu wa afya akivaa vifaa kujihadhari kuambukizwa Ebola
Wajumbe kutoka shirika la afya ulimwenguni wanakutana Geneva Uswis kuamua iwapo wautangaze mlipuko wa ugonjwa wa Ebola kama janga la barani Afrika na dharura ya dunia.

Mkutano huo unakuja wakati raia mmoja wa Saudia Arabia amefariki akiwa na dalili za ebola katika mji wa Jeddah.
Iwapo itathibitika msaudia huyo amekufa kwa ebola, kitakuwa kifo cha kwanza nje ya bara la Afrika kusababishwa na virusi vya Ebola. Arnold Kayanda na maelezo zaidi.
Tayari ugonjwa huo ambao umeenea zaidi katika eneo la Magharibi mwa Afrika umeshaua zaidi ya watu 900 kwa mwaka huu na unaonekana kuenea kwa kasi katika maeneo mengine baraani humo.
Vifo hivyo pamoja kasi ya kuambukiza huenda ikiwa kichocheo cha kulifanya shirika la Afya duniani kutangaza ugonjwa huo kuwa janga na dharura ya dunia.
Dr Ben Newman mtafiti wa masuala ya virusi katika chuo kikuu cha Reading anasema kuitangaza Ebola kama dharura ya dunia itasaidia
"Kama itakubalika hali hii kutangazwa kama suala la dharura itawaruhusu kuingia nchini na itawaruhusu kutoa msaada. Msaada kwa maana ya watu, usalama wa madaktari, na itawaruhusu kutoa misaada ya kifedha. Hiyo ni muhimu kwa sababu miundo mbinu katika baadhi ya maeneo yenye virusi haitoshi" amesema Dr Newmana.
Mbali na kutangaza ebola kuwa hali ya dharura pia shirika hilo la Afya duniani limesema kuwa mapema wiki ijayo litakuwa na mkutano wa wataalamu wa maadili ya afya kujadili uwezekano wa kutumia matibabu ya majaribio ili kudhibiti Ebola.
Tamko hilo linakuja kufuatia wamarekani wawili walioathirika na Ebola kupewa dawa hiyo 'Zmapp' na kuonekana kupata nafuu. Dr Derek Gatherer mkufunzi katika chuo kikuu cha Lancaster amesema maamuzi juu ya matumizi ya dawa ya majaribio huenda yakawa magumu.CHANZO BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...