Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, September 8, 2014

Huyu ndiye Afisa Habari Mpya wa Yanga


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiM4JiJvwvWBc09MYdb5KfXEtExMzGd5Dud1hoy0rlz0LTNkTmnAoSqQ8Ngq3bGMg0nHyOPLzafDp_1_dcE5DMGlUZ0pksxdpavvrq17aCqitx_73su2_AfgA09v4q9PKYFaT5ImPgyIFQK/s1600/jerry-muro.jpg
Jerry Muro ndiye Msemaji Mkuu wa Yanga
 MTANGAZAJI mahiri nchini aliyewahi kufanya kazi na vituo vya ITV na TBC1, Jerry Muro amekula shavu baada ya kuteuliwa kuwa Msemaji wa Yanga.
Muro anatarajia kuanza kazi ndani ya siku chache zijazo kuchukua nafasi ya aliyekuwa msemaji wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto ambaye sasa atakuwa akifanya kazi nyingine za klabu hiyo.
Muro alijipatia umaarufu mkubwa katika kuendesha vipindi vya uchunguzi akiwa ITV kabla ya kuja kuangushiwa jumba kwa kufunguliwa kesi ya Rushwa ambayo hata hivyo aliibuka kidedea dhidi ya waliomfungilia kesi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...