Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Monday, September 8, 2014

Stars bado nyanya kwa Burundi yapigwa 2-0


http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/09/stars-1.jpgTIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars bado haijapata dawa ya kufuta uteja kwa Burundi baada ya kukandikwa mabao 2-0 katika mechi ya marudiano ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa jijini Bujumbura Burundi.
Stars iliyoenda Burundi ikitamba kwenda kulipa kisasi cha mabao 3-0 ilichopewa na wenyeji wao kwenye mechi ya kirafiki ya kuadhimisha Siku ya Uhuru, ilishindwa kutimiza tambo hizo kwa kukandikwa na wenyeo wao kwenye mechi hiyo ya ugenini.
Mabao yaliyoizamisha Stars yalifungwa katika dakika ya kwanza tu ya mchezo na Saido Ntibazonkiza kabla ya Yusuf Ndikumana kuongeza la pili kwenye dakika ya 29 na kuifanya Stars ipigane kusaka angalau bao la kufutia machozi bila mafanikio yoyote.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...