Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, September 7, 2014

WAGOSI WA KAYA WAISHIKISHA ADABU POLISI MORO, WAITANDIKA 2-0 'COASTAL DAY' MKWAKWANI


TAMASHA la ‘Coastal Day’ limefanyika leo katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga ambapo mashabiki na wanachama wa klabu hiyo wamepata nafasi ya kuwaona wachezaji wapya waliosajiliwa majira ya kiangazi mwaka huu.
Coastal walioweka kambi ya mwezi mmoja kisiwani Pemba wamecheza mechi ya kirafiki na Polisi Morogoro ili kusindikiza tamasha hilo.
Afisa habari wa Coastal Union, Oscar Assenga amesema wagosi wa kaya wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu hiyo mpya ya ligi kuu msimu ujao.
Assenga alisema mabao ya Coastal Union yalifungwa katika dakika ya 35 na Ramadhan Salum aliyesajiliwa kutokea Gor Mahia ya Kenya na la pili likafungwa na Iker Bright Obina.
Baada ya mechi hiyo wachezaji wapya walitambulishwa mbele ya mkuu wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego akiambatana na mwenyekiti wa zamani wa klabu hiyo, Ahmed Aurora.

Picha za matukio ya tamasha hilo zitakujia muda wowote.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...