Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Thursday, November 6, 2014

SERIKALI YASHAULIWA KUWASAIDIA WAATHILIKA WA MADAWA YA KULEVYA


Inline image 2
Mmoja ya wasicha walioathirika na madawa ya kulevya na sasa yupo katika kituo
Inline image 3Inline image 6Inline image 7
Serikali na Taasisi zisizo za kiserikali zimetakiwa kusaidia nyumba  za malezi za waathirika wa dawa za kulevya ili ziweze kuwahudumia  watumiaji wa dawa hizo wasiokuwa na uwezo.
Ombi hilo lilitolewa jana na Frank John ambaye ni Meneja wa nyumba ya South Beach iliyopo Kigamboni kwenye hafla ya waathirika wa dawa  hizo za kulevya wanaoelelewa kwenye kituo hicho kukaa mwaka mmoja bila ya kutumia dawa za kulevya za aina yoyote ile.
“Lengo la nyumba hizi za malezi ni kupambana kuwatoa vijana hawa waliothirika na dawa za kulevya  katika hali ya uteja na kurejea katika maisha ya kawaida ili waweze kujitambua, kujiendeleza na hatimaye kutimiza ndoto zao walizokuwa nazo awali kabla hawajatumia dawa hizo.”Alisema John.
John  alisema yeye alitumia dawa hizo za kulevya kwa miaka 18 kutokana na vishawishi vya marafiki na kwamba siyo rahisi na wala haikuwa rahisi kwao  kufikisha mwaka mmoja na zaidi  bila ya kutumia dawa za kulevya za  aina yoyote bila ya kuwa na watu wa kuwasaidia na kuwaunga mkono.
Rashidi Nassoro ambaye alitumia dawa hizo za kulevya  kwa muda wa miaka sita na sasa amefanikiwa kuishi bila ya kuyatumia,  alisema mtumiaji wa dawa za kulevya ’teja’  ili aweze kupata matibabu ni gharama na kwamba matibabu yao yanachukua kipindi cha miezi minn ne na kwamba wengi wao wanashindwa.
Hivyo aliomba serikali, taasisi zisizo za kieserikali na wazazi wasiwanyanyapae, wawasaidie ili kuweza kuepuka maisha ya utumiaji wa dawa za kulevya kwa sababu ni maisha magumu, yenye vishindo na yasiyoisha mateso.
Aliongeza kuwa matibabu hayo yanawasaidia kupata nafuu ila iwaomba watumiaji waendelee kuhudhuria kwenye nyumba hizo za malezi na kuachana na marafiki wenye vishawishi ili wasije wakarejea tena kwenye matumizi hayo.
Kwa upande wa msichana  Nesha Mfinanga  alisema wamewaumiza wengi ikiwamo familia kutokana na matumizi wa dawa hizo za kulevya   na kwamba  tangu apate matibabu hayo anajitambua na kujutia makosa na muda alioupoteza wa kipindi cha miezi 9 na kuiomba jamii isiwanyanyapae iwasaidie watabadilika na kutimiza ndoto zao.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...