Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Sunday, January 18, 2015

'MANYIGU' WA KAGAME KUWAPIMA STARS MABORESHO


AMAVUBI watakaokuja nchini Januari 21 kucheza na Stars Maboresho
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiyaAxmItFj6tkllqbxqPEmTTXt_Uag1TfmwgO15zLU69HFowypQEPEV2BfzRXD9OmiAFfH9x-8Jhd73uITS4QUnhXlImCGyImYyIhZZvkk7ecs4odB6oz1o4FSCK2GJgG6yp91Ij0dkhvS/s1600/maboresho.png
Stars maboresho wanaotarajiwa kuvaana na Amavubi Januari 22
KIKOSI cha timu ya taifa ya Rwanda 'Amavubi' (Nyigu) wanatarajia kutua nchi katika kati ya wiki ijayo kuipima ubavu timu ya Taifa Stars Maboresho.
Tayari Kocha Mkuu wa Stars, Mart Nooij ameteua kikosi cha wachezaji 26 wa timu hiyo kwa ajili ya mchezo huo utakaopigwa kwenye uwanja wa CCM, Kirumba Januari 22, mwaka huu.
Nooij alisema kati ya wachezaji hao 10 ambao wanatoka katika mikoa ya kanda ya ziwa wataweka kambi Mwanza na wengine 10 wanaotoka upande wa Dar es Salaam wataweka kambi hapo Dar es Salaam.
Alisema kambi kwa ajili ya michuano hiyo itaanza rasmi kesho Jumapili  na siku inayofuata watakwenda Mwanza kuungana na wengine kwa ajili ya kambi ya pamoja.
“Mechi hiyo ni muhimu kwetu kwani wachezaji ambao watafanya vizuri tutawapandisha kucheza katika kikosi kikubwa,”alisema Nooij.
Nooij aliwataja wachezaji wa kikosi hicho kuwa ni; Aishi Manula, Benedict Tinoko, Miraji Adam, Andrew Vicent, Michael Gadiel, Emmanuel Semwanda, Joram Mgeveke, Edward Charles na Adam Salamba.
Wengine ni; Aboubakary Mohammed, Hassan Dilunga, Hussein Malombe, Shiza Ramadhani, Omari Nyenje, Kelvin Friday, Alfred Masumbakenda, Salim Mbonde, Atupele Green na Rashid Mandawa.
Pia wamo Manyika Peter, Salum Telela, Hassan Banda, Mohammed Hussein, Said Ndemla, Said Makapu na Simon Msuva.
Aidha,  kwa mujibu wa taarifa ya Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Soka Tanzani (TFF), Vedastus Lufano, kiingilio kwenye mechi hiyo itakuwa sh. 20,000 kwa viti maalumu (VIP), viti vya kawaida sh. 10,000 na mzunguko ni sh. 3,000.
Lufano aliwataja baadhi ya wachezaji wa Amavubi wanaotarajia kutua jijini Mwanza Januari 21 kwa ndege ya Rwanda Air, kuwa ni Marcel Nzarora, Olivier Kwizera, Sotel Kayomba, Ismail Nshutiyamagala , Emery Basiyenge na Michel Rushengoga.
Wengine ni Fitina Ombolenga, Janvier Mutijima, Haruna Niyonzima, Tean Baptista, Mugiraneza Savio, Nshuti Dominique, Patrick Sibomano, Jean Claude, Zagabe Andrew, Buteara Ernest , Sugira Danny, Ushengimana Betramed Iladukunda na Blenvue Mugenzi.
Lufano aliongeza kuwa taarifa iliyotumwa TFF kutoka Rwanda, Amavubi itaongozana na viongozi waliotajwa kuwa ni Stephen Costan, Vincent Mashami, Ibrahim Mugisha, Moussa Hakizimana, Nuhu Assouman, Boume Mugabe, Piere Baziki na Mkuu wa Msafara Bandora Felician.
Awali, Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) Boniface Wambura alisema mechi hiyo ni sehemu ya programu ya Kocha Mart Nooij kuiandaa timu hiyo kwa ajili ya mechi za mchujo michuano ya Afrika kwa  wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN). 
Mechi za mchujo za michuano hiyo ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Rwanda zinaanza Mei mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...