Marquee

Pata habari za Jamii,Biashara,Burudani na michezo!!

tangazo

Friday, February 27, 2015

MABONDIA WAPIMA UZITO KUZIPIGA FEB 28 UWANJA WA NDANI WA TAIFA JUMAMOSI

Mabondia Mwinyi Mzengela kushoto na Shomari Milundi wakitunishiana misuri baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao jumamosi ya kesho feb 28 utakaofanyika uwanja wa ndani wa taifa Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Fadhili Majiha akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Francis Miyeyusho utakaofanyika Feb 28 katika ukumbi wa uwanja wa ndani wa taifa Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Epson John wa Morogoro kushoto akitunishiana misuli na Vicent Mbilinyi baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao kesho utakaofanyika katika ukumbi wa uwanja wa ndani wa taifa katikati ni mratibu Antony Rutta Picha na SUPER D BOXING NEWS

Bondia Cosmas Cheka kushoto akitunishiana misuli na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa ubingwa wa U.B.O Africa utakaofanyika jumamosi ya feb 28 uwanja wa ndani wa taifa picha na SUPER D BOXING NEWS
 BONDIA IBRAHIMU  CLASS 'KING CLASS MAWE' AKIPIMA UZITO KWA AJILI YA MPAMBANO WAKE WA UBINGWA WA U.B.O AFRICA
 BONDIA FRANSIC MIYEYUSHO CHICHI MAWE AKIPIMA UZITO
Bondia Cosmas Cheka kushoto akitunishiana misuli na Ibrahimu Class 'King Class Mawe' baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa ubingwa wa U.B.O Africa utakaofanyika jumamosi ya feb 28 uwanja wa ndani wa taifa picha na SUPER D BOXING NEWS

Na Mwandishi Wetu

MABONDIA Ibrahimu Class 'King Class Mawe' na Cosmas Cheka wamepima uzito kwa ajili ya mpambano wao wa raundi kumi kugombania ubingwa wa U.B.O Africa utakaofanyika jumamosi hii katika uwanja wa ndani wa taifa
mpambano huo mkali utatanguliwa na ngumi kali kutoka kwa bondia Fransic Miyeyusho atakaezipiga na Fadhili Majiha mpambano wa raundi nane mpambano mwingine wa ubingwa ni kati ya Alibaba Ramadhani na Jacobo Maganga na katika kusindikiza mapambano hayo makali bondia machachari na chipkizi Vicent Mbilinyi ataoneshana umwamba na Epson John wa Morogoro na Shomari Milundi atapambana na Mwinyi Mzengela huku Husein Mbonde atakabiliana na Shedrack Ignas katika kuhakikisha mpambano huo unakuwa wa kihistoria na kuacha gumzo nchini bondia Said Mundi wa Tanga atapambana na Ramadhani Shauli na mapambano mengine mbalimbali

mpambano huo unaosimamiwa na P.S.T chini ya rais wake Emanuel Mlundwa yamekuwa gumzo mjini na kusababisha taflani za mabondia kutaka kupigana kavukavu uku makocha wao pia wakikunjiana ngumi

siku hiyo kutakuwa na ulinzi na usalama wa kutosha kwa watu na mali zao 


siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za ngumi  mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Ali
na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...